Hizb ut-Tahrir Kenya yafaulu kutamatisha kampeni yake Kiuchumi chini ya kauli mbiu- Msoto wa Kiuchumi Uislamu ndio Jibu.

Taarifa kwa Vyombo Vya Habari

Kwa rehema za MwenyeziMungu SWT, Harakati ya Hizb ut-Tahrir Kenya imetamatisha kampeni yake ya kiuchumi ilioanza tarehe 11 Julai 2021,na kutamatika tarehe 11 Agosti 2021.

 

Kampeni hii ilihusisha msururu wa amali; Darasa kubwa misikitini, ziara za mitaani na mazungumzo ya mitandaoni. Na katika Ijumaa ya mwisho ya mwezi mtukufu wa Dhulhijja Hizb ut-Tahrir Kenya ikagawanya toleo lililobeba anwani: ‘Mfumo muovu wa Kiuchumi wa Kibepari ndio chanzo cha Msoto wa Kiuchumi Ulimwenguni’.  ulimwenguni. Toleo hilo liligawanywa katika Miji ya Nairobi na ile ya pwani ikiwemo Mombasa, Kilifi, Malindi na Kwale.

 

Katika kipindi chote cha kampeni, Hizb ut-Tahrir/Kenya iliweza kufafanua kwa uwazi uhalisia wa mfumo muovu na potofu wa Uchumi wa Kibepari na namna ulizalisha msoto wa kiuchumi kwa umma. Kwa upande mwengine, Hizb pia ikaweka sura wazi kwa umma ya mfumo wa Kiuchumi wa Kiislamu uliotekelezwa kwa karne 13 na serikali ya Kiislamu ya Khilafah na kivitendo ukasuluhisha matatizo ya kiuchumi, sambamba na kuonyesha pia jinsi serikali hiyo ya Khilafah itakayosimamishwa hivi karibuni itakavyotatua matatizo ya kiuchumi.

 

Hashtegi za kampeni hii zilikuwa:

Kiswahili: #Msotowa_Kiuchumi_Uislamundio_Jibu

English: # EconomicHardships_IslamIsTheSolution

 

Tunamuomba MwenyeziMungu SWT atupe Khilafah chini ya mfumo wa Utume ambayo kwa hakika itakomboa walimwengu kutokana na umasikini uliozaa. Na mwisho wa dua zetu ni kwa sifa njema zote zinamstahiki MwenyeziMungu bwana wa walimwengu wote.

Shabani Mwalimu

Mwakilishi kwa Vyombo Vya Habari

 Hizb ut Tahrir Kenya

REF: 1443/001

JUMATANO 03 MUHARRAM  1443 AH

11/08/2021 CE